• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maulizo |
    • Barua pepe |
Longido District Council
Longido District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Longido

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya jamii
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Afya
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Usafishaji na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
        • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Teknolojia ya habari, mawasiliano na uhusiano
      • Ukaguzi wa ndani
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu ,afya na Maji
      • Kamati ya kuthibiti Ukimwi
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili ya madiwani
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • miradi iliyokamilishwa
  • Machapisho
    • sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • mpango mkakakati
    • Riport mbalimbali
    • Form mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MITUNGI 50 YATOLEWA KWA BABA NA MAMA LISHE WILAYANI LONGIDO

Posted on: April 17th, 2025

Na Happiness Nselu , Longido

Katika juhudi za serikali ya awamu ya sita kuhamasisha matumizi ya nishati safi na kuondokana na utegemezi wa nishati chafu kama kuni na mkaa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametoa msaada wa mitungi 50 ya gesi kwa mama na baba lishe wa Wilaya ya Longido.

Zoezi la ugawaji wa mitungi hiyo limefanyika kwa mafanikio makubwa na kuongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Longido, Mhe. Salum Kalli, ambaye alikabidhi rasmi mitungi hiyo kwa wajasiriamali hao wadogo kama sehemu ya mpango wa kitaifa wa matumizi ya nishati safi kwa ajili ya kuhifadhi mazingira na kuboresha afya za wananchi.

Akizungumza wakati wa tukio hilo, Mhe. Kalli alisema kuwa dhamira ya Rais ni kuhakikisha kila kaya, hasa zinazojihusisha na shughuli za upishi, zinatumia nishati safi ili kuokoa mazingira na kupunguza athari za kiafya zitokanazo na moshi wa kuni na mkaa.

“Rais amedhamiria kuona Watanzania wanapika kwa usalama zaidi na kwa njia ya kisasa. Mitungi hii ya gesi si tu kwamba itarahisisha kazi zenu, bali pia ni mchango mkubwa katika mapambano dhidi ya uharibifu wa mazingira,” alisema Mhe. Kalli.

Afisa Maendeleo ya Jamii wa Wilaya hiyo, Bi Grace Mghase, alitumia fursa hiyo kuwahimiza wakazi wa Longido kuunga mkono juhudi za serikali kwa kubadilika kifikra na kuachana na matumizi ya nishati chafu.

“Hii ni fursa muhimu kwa jamii yetu. Tukiendelea kutumia kuni na mkaa, tunaharibu misitu na afya zetu pia ziko hatarini. Gesi ni njia salama, safi na ya haraka katika shughuli za kila siku, hasa kwa mama na baba lishe ambao muda ni rasilimali muhimu,” alieleza Bi Mghase.

Kwa upande wake, mama Saruni ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Mama na Baba Lishe wilayani humo, alitoa shukrani kwa serikali kwa kuwakumbuka wafanyabiashara wadogo na kuwapatia vifaa vinavyowawezesha kuboresha huduma zao kwa wateja.

“Kwa kweli tumefurahi sana. Hatua hii ni ya kihistoria kwa sisi mama na baba lishe wa Longido. Tunaahidi kuzitumia mitungi hii kwa uangalifu, tukiwa na lengo la kuboresha huduma zetu na kuhakikisha wateja wetu wanapata vyakula bora kwa wakati,” alisema mama Saruni kwa furaha.

Wananchi waliohudhuria tukio hilo walionekana wenye hamasa kubwa huku wengi wakisema kuwa hatua hiyo imewapa mwanga kuhusu umuhimu wa kuhama kutoka kwenye matumizi ya kuni na mkaa kwenda kwenye nishati safi kama gesi, jua, na umeme wa uhakika.

Kwa mujibu wa Afisa Maendeleo ya Jamii, mpango wa ugawaji wa nishati safi utaendelea kutekelezwa kwa awamu mbalimbali, huku vikundi vya wajasiriamali, mashule, na taasisi za kijamii vikipewa kipaumbele katika mgao wa vifaa hivyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10% January 30, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 09, 2023
  • Uchaguzi wa kidato Cha tano 2023 June 11, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2023
  • View All

Habari Mpya

  • MITUNGI 50 YATOLEWA KWA BABA NA MAMA LISHE WILAYANI LONGIDO

    April 17, 2025
  • WATAALAMU WA AFYA WATOA ELIMU KUHUSU MPOX KATIKA SHULE YA SEKONDARI ENGARENAIBOR NA KETUMBEINE

    March 21, 2025
  • WWF NA BBC MEDIA ACTION WATOA MAFUNZO KWA VIONGOZI WA JAMII JUU YA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    March 21, 2025
  • IDARA YA AFYA ,USTAWI WA JAMII NA LISHE YAADHIMISHA SIKU YA AFYA YA KINYWA NA MENO

    March 21, 2025
  • View All

Video

Ujenzi wa madarasa 4 na Ofisi ya walimu shule shikizi Lopoloseki,
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Ufugaji
  • Elimu msingi Primary Education

Kurasa za zinazoshabihiana

  • Tovuti kuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa wa Arusha

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Arusha- Namanga Road, Longido Town

    Postal Address: S.L.P 84 Longido Arusha

    Telephone: 027-2539603

    Mobile: 0756395889

    Email: ded@longidodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maulizo
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2016 Longido DC . All rights reserved. Designed by Loth Zacharia & Joseph Peter Mkumbwa Sponsored by GWF TAMISEM